Edit Content

About Us

TAMWA is a national level Non-Governmental Organization known as Tanzania Media Women’s Association formed in 1987. TAMWA Zanzibar became fully self-governing and operational in both Isles of Unguja and Pemba since 2004. In January 2007, it attained its own separate registration.

Contact Info

TAMWA-ZNZ yaomba mkakati wa kitaifa kubadilisha tabia kwa vijana

TAMWA-ZNZ yaomba mkakati wa kitaifa kubadilisha tabia kwa vijana

TAMWA-ZNZ yaomba mkakati wa kitaifa kubadilisha tabia kwa vijana.

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kinashauri kuandaliwa kwa mkakati wa kitaifa wa kubadilisha tabia za vijana ili kuwanusuru na kutumbukia katika vitendo vya udhalilishaji. 

Kwa mujibu wa Afisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar kuanzia Julai mpaka Septemba, 2023 ni kwamba watu 24 wamekutwa na hatia mahakamani kwa kufanya makosa ya udhalilishaji na kupewa adhabu za vifungo (kwa Zanzibar huitwa vyuo vya mafunzo) ambapo asilimia 58.3 ni vijana wa umri wa 18-29.

Hii ni kwamba, vijana wamekua wakijihusisha sana na masuala ya udhalilishaji na hivyo jitihada za makusudi zinahitajika ili kuwabadilisha mawazo ili kutotumbukia katika majanga haya kwa maslahi yao, watoto na nchi kwa jumla. 

Takwimu hizo pia zinaonesha watu ambao bado wapo mahabusu kesi zao zinaendelea ni 48 ambapo kundi hilo la miaka 18 hadi 29 pia linaongoza ambalo linafanya asilimia 54.

Tunaishauri Serikali kuandaa mkakati wa kuelimisha vijana kupitia maeneo mbalimbali ikiwemo viwanja vya michezo, skuli lakini pia kutoa taaluma kwa wazazi na walezi jinsi ya kuwafahamisha watoto wa kiume namna ya kuheshimu watoto wa kike, wanawake na watoto kwa jumla.

Takwimu pia zinaonesha kuwa masuala hayo ya udhalilishaji yanawaathiri watoto zaidi ambapo katika matukio 157 kwa mwezi Julai hadi Septemba yaliyoripotiwa, watoto ni 122 sawa na asilimia 77 katika maeneo kadhaa hasa kubakwa, kakashifiwa na kulawitiwa.

TAMWA ZNZ pia inawashauri sana vijana kushtushwa na taarifa hizi na hivyo kujipangia mipango madhubuti ya kutokuingia katika vitendo hivi ikiwemo kuacha kufuata vishawishi, kutokuendekeza mihemuko na pia kujidhibiti dhidi ya matumizi mabaya ya mitandao.

Ni vyema vijana wakaelewa kuwa katika vijana hao waliotiwa hatiani wengi wao wamehukumiwa kutumikia adhabu ya miaka 11 na zaidi hivyo kupoteza kipindi kirefu cha nguvu zao katika vyuo vya mafunzo badala ya kutumia kujipanga na maisha yao. 

TAMWA ZNZ pia imefarijika sana na Afisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutoa takwimu zinazoonyesha mgawanyiko wa umri wa waliofanya uhalifu ikiwemo makosa ya udhalilishaji.

Utoaji huu wa takwimu utasaidia kujua umri wa wafanyaji wa makosa mbalimbali na hivyo kuona jinsi gani nchi inaweza kujipanga katika kubadilisha tabia za makundi yaliyo hatarishi zaidi.

Dkt. Mzuri Issa,
 Mkurugenzi,
TAMWA ZNZ.
****************************************************************************************************************

TAMWA-ZNZ calls for a national strategy to change the behavior of youth

TANZANIA Media Women’s Association, Zanzibar (TAMWA-ZNZ), recommends the preparation of a national strategy to change the behavior of young people, aiming to prevent them from engaging in acts of humiliation.

According to the Office of the Chief Government Statistician (OCGS) in Zanzibar, from July to September 2023, 24 people have been convicted by courts of laws and sent to prisons, locally known as rehabilitation centres of which 58.3 percent are young people aged 18-29. 

This data suggests that young people have become significantly involved in sexual abuse calling for behavioural change program to shift their mindset and prevent them from participating in these tragic activities, which affect their well- being, children, and the country in general.

The statistics also reveal that 48 people are still in custody, with their cases ongoing while the age group; 18 to 29-year-old, a tender age group, and of course, productive age is in the lead again by 54 percent.

We strongly advise the government to formulate a strategy for educating young people through various means, including playgrounds, schools and at households encouraging parents and guardians to teach male children about respecting girls, women, and children in general.

The statistics also highlight that children are disproportionately affected by acts of humiliation, with 77 percent of the 157 reported cases from July to September involving children. These incidents often relate to rape, defamation, insults, and sodomy.

TAMWA ZNZ urges young people to take this information seriously and plan not to engage in such actions. This includes resisting temptations, controlling their        emotions,        and        using       social       networks        responsibly. It is essential for young people to understand that many of those convicted are sentenced to more than 11 years in prison, which means they waste a significant portion of their lives behind bars rather than using their energy to improve their lives.

TAMWA ZNZ also appreciates/nods the Office of the Chief Statistician of the Revolutionary Government of Zanzibar for providing statistics that reveal the age distribution of those who commit crimes, particularly those related to humiliation and violence. These statistics will help identify the age groups most vulnerable to such behavior and enable the country to develop strategies for positive change.

Dr. Mzuri Issa,
Director,
TAMWA ZNZ.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Subscribe to our
News and Presses

***We Promise, no spam!

A national level Non-Governmental Organization known as Tanzania Media Women’s Association formed in 1987.The registration number is 493 under Zanzibar Society Act No. 6 of 1995

We’re Available

Monday : 08.00 - 10.00
Tuesday : 08.00 - 10.00
Wednesday : 08.00 - 10.00
Thursday : 08.00 - 10.00
Friday : 09.00 - 07.00
Saturday : 10.00 - 05.00
Sunday : 10.00 - 05.00