Edit Content

About Us

TAMWA is a national level Non-Governmental Organization known as Tanzania Media Women’s Association formed in 1987. TAMWA Zanzibar became fully self-governing and operational in both Isles of Unguja and Pemba since 2004. In January 2007, it attained its own separate registration.

Contact Info

JESI LA POLISI LATAKIWA KUHARAKISHA UPELELEZI TUKIO LA KUVAMIWA KWA MWANAHARAKATI

JESI LA POLISI LATAKIWA KUHARAKISHA UPELELEZI TUKIO LA KUVAMIWA KWA MWANAHARAKATI

12/6/2024


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


JESI LA POLISI LATAKIWA KUHARAKISHA UPELELEZI TUKIO LA KUVAMIWA
KWA MWANAHARAKATI
Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) pamoja na Chama cha Waandishi wa
habari Wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA ZNZ) inaliomba Jeshi la Polisi nchini
kuharakisha upelelezi wa kuvamiwa nyumbani kwake Mwanaharakati Amina Yusuf Ramadhan,
siku ya Alhamis tarehe 23/5/2024 majira ya usiku, Fuoni Mambosasa Wilaya ya Magharibi
“B” Unguja.
Kwa mujibu wa muathirika watu hao wawili wakiume waliovaa maski usoni walivamia na
kuvunja mlango wa nyumba ya mwanaharakati huyo huko Fuoni Mambosasa na kuiba TV ya
inchi 53,DVD, pasi, Komputa Mpakato (laptop) ,pamoja na nakala za taarifa, vitu vyote vikiwa
na thamani ya Shilingi milioni mbili na laki mbili za Kitanzania.
Pia watu hao walimjeruhi Bi Amina na kumsababishia kupata maumivu makali sambamba na
kujenga hofu kubwa na kuathiri uwezo wake wa kuendelea na maisha ya kawaida. Tukio hilo
liliripotiwa katika kituo cha Polisi Fuoni kwa Fuo R/B 968/2024: Fuo IR 45/2024- 25/05/2024.
ZAFELA na TAMWA – ZNZ zimesikitishwa sana na tukio hilo na inalaani kitendo hicho
alichofanyiwa Bi Amina ambaye ametoa mchango mkubwa katika mapambano ya vita dhidi ya
udhalilishaji.
“Tunasikitika kuwa hali kama hii inaweza kutishia wanaharakati wengine kuendelea na kazi zao
pamoja na yeye mwenyewe bi Amina na hivyo kuzorotesha hali ya ufuatiliaji wa masuala ya
kidhalilishaji na ukatili nchini”.
TAMWA ZNZ na ZAFELA tunaliomba Jeshi la Polisi kuharakisha upelelezi wa tukio hilo kwa
vile ndicho chombo pekee chenye dhamana hiyo na kutoa taarifa kwa jamii ili kuhakikisha
wanawakamata wote wanaohusika na tukio hilo kuwafikisha katika vyombo vya sheria.Sambamba na hilo vyombo vinavyosimamia sheria nchini tunaviomba kuyachukulia matukio
kama haya kwa uzito mkubwa kwa vile wanaharakati pamoja na wananchi na watu wengine
wote wana haki ya kulindwa usalama wao na mali zao.
“Ipo haja ya kufanyakazi kwa ufanisi ili kuhakikisha kuwa wahalifu wanawajibishwa kwa
vitendo vyao, hali hii inajenga imani kwa jamii juu ya vyombo vinavyosimamia sheria na
itasaidia kujenga jamii iliyo sawa bila ya ubaguzi ama upendeleo wowote.
ZAFELA na TAMWA ZNZ zinaamini kwamba Jeshi la Polisi lina uwezo mkubwa wa
kukomesha matukio ya ukatili na kuvamiwa kwa wanawake na makundi mengine Zanzibar na
zipo tayari kutoa mashirikiano pale inapohitajika.
Imetolewa na ZAFELA na TAMWA – ZNZ
Jamila Mahmoud
Mkurugenzi
ZAFELA
Dr. Mzuri Issa
Mkurugenzi
TAMWA ZNZ


Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxzxxxxxxxxxxxxxxxx
PRESS RELEASE
POLICE URGED TO EXPEDITE INVESTIGATION INTO ACTIVIST ATTACK
The Zanzibar Female Lawyers Association (ZAFELA) and the Tanzania Media Women’s
Association Zanzibar (TAMWA ZNZ) are calling on the police force to expedite the
investigation into the attack on activist Amina Yusuf Ramadhan, which occurred on Thursday
night, May 23, 2024, at her home in Fuoni Mambosasa, West District “B” Unguja.
According to the victim, two masked men broke into her home, stealing a 53-inch TV, DVD
player, iron, laptop, and various documents, with the total value estimated at 2.2 million
Tanzanian shillings.
Additionally, the assailants inflicted severe injuries on Ms. Amina, causing her pain and creating
a substantial fear that has affected her ability to continue with her daily life. The incident was
reported at the Fuoni Police Station under reference number Fuo R/B 968/2024: Fuo IR 45/202425/05/2024.
ZAFELA and TAMWA ZNZ are saddened by this incident and condemn the attack on Ms.
Amina, who has made significant contributions to the fight against abuse.
“We are concerned that such incidents may discourage other activists from continuing their
work, including Ms. Amina herself, thereby hindering the efforts to combat abuse and violence
in the country.”TAMWA ZNZ and ZAFELA urge the police to expedite the investigation, as they are the only
body/organization mandated to do so, and to keep the public informed to ensure that those
responsible are apprehended and brought to justice.
Furthermore, we call on the legal authorities to take such incidents seriously, as activists,
citizens, and all individuals have the right to protection and security for themselves and their
property.
“It is crucial to work efficiently to ensure that criminals are held accountable for their actions.
This builds public trust in the legal system and helps to create social justice without
discrimination or favoritism.”
ZAFELA and TAMWA ZNZ believe that the police force has the capability to control violence
and attacks against women and other groups in Zanzibar, and we are ready to provide support
whenever needed.
Issued by ZAFELA and TAMWA ZNZ


Jamilla Mahmoud
Director,
ZAFELA


Dr. Mzuri Issa
Director,
TAMWA ZNZ

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Subscribe to our
News and Presses

***We Promise, no spam!

A national level Non-Governmental Organization known as Tanzania Media Women’s Association formed in 1987.The registration number is 493 under Zanzibar Society Act No. 6 of 1995

We’re Available

Monday : 08.00 - 10.00
Tuesday : 08.00 - 10.00
Wednesday : 08.00 - 10.00
Thursday : 08.00 - 10.00
Friday : 09.00 - 07.00
Saturday : 10.00 - 05.00
Sunday : 10.00 - 05.00